NA: DIANA ELIAS, FJS
Wanawake nchini Tanzania wametakiwa
kutumia njia salama za uzazi wa mpango na kujiepusha na matumzi ya vidonge vya (P2) vinavyotumika kuzuia Mimba kwani vinaweza kusababisha kutopata mtoto (ugumba)
kama vikitumiwa bila ushauri wa madaktari.
Akizungumza na maipac media
Tanzania, Dk. Daniel
Godwin wa maabara ya Usanda iliyopo jijini Arusha jana Julai 27,2023 amesema kuwa matumizi
makubwa ya vidonge vya (P2) kwa wanawake huenda ukasababisha ugumba kwa mtoto wa
kike vikitumiwa bila uangalifu.
Amesema (P2) ni vidonge vinavyo tumika
kuzuia Mimba au kuharibu mfumo wa kupata mimba na madhara yake ni pamoja na
kuharibu mfumo wa hedhi, kuvuruga homon, kuharibu kuta za uzazi na kusababisha
ugumba.
Dkt.
Godwin amewashauri wanawake au wasichana kutumia njia zingine za uzazi wa
mpango au kuepuka mimba zisizo tarajiwa ikiwemo kutumia kalenda na mipira ya
kiume na kike ili kuzuia mimba na magonjwa ya zinaa kuliko kutumia vidonge
ambavyo madhara yake ni makubwa.
Vilevile
amewashauri wanawake au wasichana wasizidishe matumizi ya p2 kama njia ya
kuzuia mimba zisizo tarajiwa kwasababu dawa hizo zina madhara kwa afya zao.
Doreen
Godfrey (22) mkazi wa kwa mrombo jijini Arusha amesema ajuavyo yeye madhara ya
matumiazi ya vidonge vya P2 kwa akina mama ni pamoja na kutokuona siku za hedhi
kwa wakati au kwa mpangilio na wakati mwingine kutokuona kabisa siku zao kwa
miezi kadhaa.
Kwaupande
wake Joyce Isaya (27) mfanyabiashara wa duka la vipodozi maeneo ya kwa mrombo
jijini Arusha amesema wanawake wengi Wanatumia p2 bila kujua madhara yake hivyo
elimu kuhusu madhara ya vidonge hivi na baadhi ya njia za uzazi wa mpango zingetolewa
kwa ukubwa ili wanao tumia njia hizo wajue namna ya kuepuka madhara hayo.
Sambamba
na hayo ameeleza njia zingine ambazo ni salama ili kuepuka mimba zisizo tarajiwa
ni kutumia kalenda na mipira ya kiume na kike wakati wa kujamiiana ambayo
itazuia mimba pamoja na magonjwa ya zinaa kama kisonono, kaswende na ukimwi.

No comments:
Post a Comment