Watu kadhaa wanahofiwa kufariki dunia katika ajali iliyotokea eneo la Kibaoni Ngaramtoni, wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha ikihusisha magari matatu kugongana.
Kwa munibu wa mashuhuda wanasema Chanzo cha ajali hiyo ni baada ya gari lililokuwa limepakia mtambo wa mashine ya kutengeneza barabara kuacha njia na kuparamia magari matatu ambayo ni Coster, Haice na gari ndogo binafsi lililokuwa imepakia raia wa kigeni ambao wawili kati yao wanahofiwa kufariki dunia eneo la tukio.
Miili ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha maiti katika hospitali ya Rufaa ya Mt Meru ,huku majeruhi wakipelekwa kupatiwa matibabu katika hospitali ya ALMC na Mount Meru.
Endelea kuwa nasi Kwa Taarifa zaidi
No comments:
Post a Comment