HIFADHI YA TAIFA BURIGI-CHATO IPO TAYARI KUPOKEA WATALII - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Friday 9 February 2024

HIFADHI YA TAIFA BURIGI-CHATO IPO TAYARI KUPOKEA WATALII



Mkuu wa hifadhi Chato- Burigi, Kamishna Msaidizi Ismaili Omari akizungumza na waandishi wa Habari 





Mwandishi wetu, MAIPAC


maipacarusha20@gmail.com


Hifadhi ya Taifa ya Burigi -Chato, Sasa ipo tayari kupokea maelfu  ya watalii baada ya Shirika la hifadhi za Taifa (TANAPA) kukamilisha miundombinu ya barabara na mawasiliano ambayo awali ilikuwa ni shida.


Hifadhi hii iliyonzishwa mwaka  2019, kiasi cha sh bilioni  3.3 tayari zimetumika kuimarisha miundombinu yake ili watalii wa ndani na nje waweze kutembelea.


Mkuu wa hifadhi hiyo, Kamishna Msaidizi Ismaili Omari  akizungumza na waandishi wa habari za Utalii na Uhifadhi waliotembela hifadhi hiyo, alisema wanaalika watalii kutoka ndani na nje ya nchi kutembelea hifadhi hiyo.


" Shirika la hifadhi za Taifa (TANAPA ) limefanya maboresho makubwa ya Miundombinu na kazi inaendelea lakini pia Kampuni ya simu  ya TTCL imeweka mnara wa Mawasiliano hifadhini "amesema 



Mhifadhi Omar alisema barabara zenye urefu wa kilomita 97.5 pamoja na madaraja na vivuko yamejengwa lakini pia sasa umekamilika ujenzi wa kambi za Utalii na makazi ya bei nafuu ya watalii ndani ya hifadhi .


 "Lakini pia tunahifadhi mazingira na uoto wa asili na Sasa wanyamapori wameongezeka na wanaonekana kirahisi" amesema



Afisa utalii hifadhi ya Burigi- Chato, Aldo Mduge amesema upekee wa hifadhi hiyo ni uwepo wa ndege aina ya Domo kiatu (African Shoebill) maziwa yanayo zunguka hifadhi  wanyama wengi na ndege aina 400.


Mduge amesema hivi Sasa kuingia katika hifadhi hiyo ni rahisi kwa usafiri wa barabara, Anga na kupitia Maji .


"Awali kulikuwa na changamoto lakini Sasa hifadhi inafikika maeneo yote na tuna vivutio vingi ikiwepo wanyama wa kubwa kama Tembo, Simba, Chui, Nyati, Twiga na wengine "amesema 


Akizungumzia makazindani ya hifadhi, Kaimu mkuu idara ya utalii hifadhi  hiyo, Emmanuel Nyundo hiyo alisema uwekezaji walio ufanya ikiwemo kujenga kambi ya wageni ya kudumu huku  akiwakaribisha   wageni kuwekeza katika hifadhi hiyo kwani kuna maeneo mazuri.


"Kuna maeneo ya ujenzi wa kambi za Utalii, mahoteli na vivutio vingine vya Utalii"amesema


Hifadhi hii  ina kilomita za mraba 4707 katika wilaya za Biharamulo, Chato, Karagwe ,Ngara na Muleba ipo katika mikoa ya Kagera na Geita.


No comments: