RAIA WA BURUNDI 12 WASHIKILIWA KWA KUINGIA BILA KIBALI NCHINI - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Wednesday 11 September 2024

RAIA WA BURUNDI 12 WASHIKILIWA KWA KUINGIA BILA KIBALI NCHINI

 

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Alex Mkama


Na Lilian Kasenene, Morogoro


maipacarusha20@gmail.com


RAIA 12 wa Burundi wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro kwa  tuhuma ya kuingia nchini bila kibali.


Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Alex Mkama alisema hayo jana mjini hapa wakati akitoa taarifa  ya mafanikio katika oparesheni zinazoendelea ambazo zinalenga kutanzua na kuzuia uhalifu mkoani hapo.


Kamanda huyo aliwataja waliokamatwa ni Tusenge Juvenal(25),Nshimumukiza Eloje (20), Nibizi Elia (30),Nduwayo Ally (21), Niyomwungere Jabal (18), Nimbona Pierre (34), Ndayishimye Jean (20), Kamaliza Geraridine (28), Niyonizeye Sandrine (8), Kezakimana Lidia (6), Miburo Malitha (4),na Josefu Nikora (14)


Aidha alisema watuhumiwa wote wamekamatwa Septemba 4, 2024 huko kata ya Dakawa Wilaya ya Mvomero  wakiwa wanafanya kazi katika mashamba ya miwa .


"Mafanikio hayo ni pamoja na kukamata watuhumiwa wanaojihusisha na matukio mbalimbali ya uhalifu ikiwemo wizi wa mifugo, usimamizi wa kesi mahakamani na oparesheni za usalama barabarani. "alisema.


"Oparesheni hii imefanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa wawili  wengine wawili wanaojihusisha na matukio ya ujambazi katika maduka"alisema.


 Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni  waliokamatwa ni Joseph Kusekwa (55) mkazi wa Mgudeni ambaye alikamatwa akiwa na mali za duka zilizoibiwa katika duka la  Leonard Mhina (40) mfanyabiashara  mkazi wa Mnyunywe kata ya Maguha Wilaya Kilosa. 


Alisema  katika Wilaya ya Kilombero 

alikamatwa Jofrey Sixbert (21) mkazi wa Kiberege aliyekuwa anatafutwa kwa matukio ya ujambazi akiwa na mali mbalimbali za wizi ambazo ni Simu, TV, Sabufa na funguo 70 zinazofungua milango mbalimbali. 


Aidha alisema mafanikio yamepatikana katika doria na misako dhidi ya wezi wa mifugo ambapo Septemba 7, 2024 katika kijiji cha Msolwa kata ya   Ruhembe Jeshi la Polisi lilifanikiwa walikamatwa watuhumiwa watatu ambao ni wezi  wa mifugo. 


Watuhumiwa wengine walikamatwa Septemba 3, 2024 wakiwa na nyama ya ng’ombe  zilizochinjwa baada ya kuiba ng’ombe 14 mali ya Lucas Kazimoto .


Aliwataja watuhumiwa walikutwa wakiuza nyama ya ngo’ombe, ikiwa ni sehemu ya ile iliyoibwa

Waliokamatwa ni Yohana Sambuka Mliga (22) mkulima mkazi wa Zombo Christian Damian Mgomi (41) mkazi wa Madizini, Mohamed Kibwana Mnazi (40) mkulima mkazi wa Madizini, Christian Damian Mgomi (41) mkazi wa Madizini wilayani Mvomero .


Wakati huo huo kamanda huyo alisema . madereva wanne (4) wamefungiwa leseni zao na kati ya hao wawili (2) wamefikishwa mahakamani kwa makosa ya usalama barabarani ikiwemo mwendokasi.


Alisema oparesheni ya usalama barabarani imehusisha ukamataji wa pikipiki 52 na bajaji 22 zinazojihusisha na uhalifu. Miongoni mwa pikipiki hizo ni zile zinazokatwa bomba la moshi ambazo husababisha kelele zinapopita barabarani. 


Aidha, waendeshaji wasio na leseni wametakiwa kujiunga na mafunzo ya udereva kabla ya kuadhibiwa.


Mwisho.

No comments: