MAKONDA AWAAGIZA MADIWANI JIJI LA ARUSHA KUELEZEA KWA WANANCHI MIRADI ILIYOTEKELEZWA KWA UFASAHA - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Saturday, 21 June 2025

MAKONDA AWAAGIZA MADIWANI JIJI LA ARUSHA KUELEZEA KWA WANANCHI MIRADI ILIYOTEKELEZWA KWA UFASAHA

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh.Paul Makonda akiwa na madiwani wa Jiji la Arusha waliomaliza muda wao wakijiandaa kwa Uchaguzi Mkuu ujao


Na Queen Lema, Arusha 


maipacarusha20@gmail.com 


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh.Paul Makonda amewaomba madiwani pamoja na watendaji wa halmashauri ya jiji la Arusha kuwa mabalozi wazuri wa kuelezea miradi mikubwa ambayo imetekelezwa na serikali 


Aidha endapo watu kama waliokuwa  madiwani wataenda Kuelezea kwa wananchi Kwa ufasaha kabisa miradi iliofanyika itaweza kuruhusu  wananchi kuendelea kuiamini serikali yao.


Makonda ameyasema hayo Leo wakati akifunga rasmi baraza la madiwani WA jiji la Arusha ambapo pia makonda alitumia mkutano huo kuweza kutoa shukurani kwa madiwani pamoja na aliyekuwa meya WA jiji la Arusha Max Iraqhe.


 Alisema ni wakati sahihi sasa wa kuhakikisha kuwa kila aiyekuwa diwani  wa baraza Hilo anasemea vyema miradi ikiwa ni pamoja na kusema thamani halisi ya miradi hiyo.


"Tuwe wazalendo na nchi yetu lakini pia tuhakikishe kuwa Yale tulioyaona lakini pia kuyafanya na kupitisha bajeti humu ndani na kisha yakatekelezwa basi tuyaseme tena hadharani kila Mtu aweze kuyajua na kutambua "aliongeza Makonda



No comments: