MWANASHERIA MKUU ARIDHISHWA NA KASI UTENDAJI KAZI WA WANASHERIA. - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Tuesday, 28 April 2026

MWANASHERIA MKUU ARIDHISHWA NA KASI UTENDAJI KAZI WA WANASHERIA.

 

Mwanasheria mkuu wa Serikali Hamza Johari
 


 


Na Queen Lema,Arusha


maipacarusha20@gmail.com 


Mwanasheria mkuu wa Serikali Hamza Johari amewataka watumishi wa ofisi  yake  pamoja na wadau wengine wa sheria kuhakikisha kuwa wanaisoma vyema Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050 na kuielewa ipasavyo kwani ofisi yake inatakiwa kutekeleza Dira hiyo kwa asilimia zote


Mbali na kuisoma na kuielewa ipasavyo Dira hiyo pia wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii zote 


Mwanasheria huyo ameyasema hayo Jijini Arusha wakati akizungumza kwenye baraza la wafanyakazi wa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali mapema leo.


Johari alisema kuwa dira ya mwaka 2050 ya maendeleo inalenga kuinua taifa lakini pia ili dira hiyo iweze kuwanufaisha sekta ya sheria inatakiwa kila mmoja aweze kuzisimamia ipasavyo


"Dira ya 2050 sisi ni washiriki tena wakubwa natumia jukwaa hili kuwahimiza kila mmoja aisome aielewe lakini pia muhakikishe kuwa mnawajibika ipasavyo kwenye masuala ya sheria"aliongeza.

Wanasheria wa Serikali

Wakati huo huo aliwataka wafanyakazi wa ofisi hiyo kuhakikisha kuwa wanafanya kazi kwa kuzingatia malengo ya ofisi.


"Malengo  yetu pamoja na vipaumbele tulivyoweka kama Taasisi vinatakiwa kufanyiwa kazi kila kazi nzuri tunayoifanya kwa kushirikiana inaruhusu hata ongezeko kubwa la bajeti  ya ofisi yetu"  aliongeza


Naye Mwenyekiti wa Tughe ,Baraza la wafanyakazi ofisi ya mwanasheria mkuu wa Serikali Rashid Kigalu, alisema kuwa wao kama watumishi wa ofisi hiyo  wanashukuru Ofisi yao kwa kuweza kuwapa fursa mbalimbali kama vile  mafunzo Sekta ya Afya,pamoja na mafunzo ya ndani  ya uwajibikaji wao 


Kigalu alisema kuwa fursa hizo zimeweza kuruhusu uwajibikaji wa hali ya juu hali ambayo imeleta hata ongezeko kubwa la bajeti ya ofisi hiyo.

No comments: