Na Mwandishi wetu,Arusha
maipacarusha20@gmail.com
Chama Cha mapinduzi mkoa wa Arusha kinatarajia kumpokea Katibu wa itikadi uenezi na Mafunzo,Kenani Kihongosi ambapo atafanya ziara kwenye wilaya tatu za mkoa wa Arusha kuanzia June 4
Akizungumza na waandishi wa habari mapema Leo Katibu wa Siasa na uenezi mkoa wa Arusha ,Bw Saipulani Ramsey Alisema kuwa watampokea kiongozi huyo ambaye atakuwa Arusha kwa muda wa siku 3
Alisema kuwa Kenani anafanya ziara zake kote nchini ikiwa ni mkakati maalumu wa Ccm baada ya kukamilika kwa uchaguzi mkuu.
Alifafanua kuwa Kenani ataanzia ziara yake June nne katika wilaya ya Karatu,June 5 atakuwa Arumeru,na siku ya June 6 atakuwa Arusha mjini
"Lengo la kuzunguka kw a kiongozi huyo ni kukutana na wananchi lakini pia kukagua miradi mbalimbali ambayo inatekelezwa na Serikali"aliongeza
Katika hatua nyingine alisema kuwa wananchi wanatakiwa kujitokeza kwa wingi sana lakini pia hata kutoa madukuduku yao ambayo wanayo
"Kwenye hizi wilaya ambazo zitakuwa na ugeni huu wa Kitaifa tunawasihi sana wananchi waje kusikiliza hoja za Ccm ,walete yale ambayo yanawakwamisha au yameshindwa kutekelezwa ipasavyo,na miradi inayotekelezwa na niya wananchi hivyo wajitokeze"aliongeza
Akiongelea utendaji kazi wa Ccm mkoa wa Arusha alisema kuwa mkoa umeweza kufanya ziara katika kata 101 katu ya kata 161
"Baada ya uchaguzi mkuu huwa tunafanya tathimini kwa wananchi wetu,na tumeshamaliza kata hizo zilizobaki Bado tutahakikisha kuwa tunazifikia ikiwa ni pamoja na kuangalia changamoto zilizopo ndani ya kata hizo"aliongeza.
Alihitimisha kwa kusema kuwa kwa kipindi kilichopita Cha uchaguzi mkuu Ccm ilifanikiwa kushinda kwa asilimia zaidi ya 98 na kwa uchaguzi ujao wa mwaka 2030 wanatarajia kufikia asilimia 100.

No comments:
Post a Comment