Dkt Johannes Lukumayi afanya ziara na Kutatua kero za wakazi wa kata za mwandeti na Musa Wilayani Arumeru - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Friday, 17 July 2026

Dkt Johannes Lukumayi afanya ziara na Kutatua kero za wakazi wa kata za mwandeti na Musa Wilayani Arumeru

 



Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi Dkt Johannes Lukumayi akisikiliza kero za wananchi wa Mwandeti



 


Na Mwandishi wetu, Arusha 


maipacarusha20@gmail.com 



Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi Dkt Johannes Lukumayi ametembelea vijiji mbalimbali vya kata ya mwandeti, pamoja na Musa, na kisha kukagua miradi mbalimbali ya maendeleleo inayotekelezwa na Serikali 


Mbali na mbunge huyo kufanya ziara katika kata hizo pia mbunge huyo amesikiliza na kutatua changamoto mbalimbali zilizopo kwenye kata hizo


Akiongea na maelfu ya wananchi waliodhuria katika mikutano ya hadhara ya mbunge huyo alisema kuwa mara baada ya kuchaguliwa na wananchi alipata pia ridhaaa ya kuwa na nyadhifa mbalimbali za bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania


Aliwashukuru wananchi wa mwandeti kwa kuweza kumpatia kura nyingi yeye pamoja na Raisi Samia suluhu pamoja na diwani wa kata hiyo 


Alisema kuwa kupitia kura nyingi Sana ambazo zimetoka kwenye kata ya Mwandeti alisema Serikali itaendelea kuboresha miradi mbalimbali hasa ya kijamii


Dkt Lukumay alisema kuwa mwandeti pamoja na Musa ina wananchi wengi ambao wanajitoa sana kwenye masuala ya maendeleleo na hivyo yeye atahakikisha kuwa anasimamia maitaji yote ndani ya kata hiyo 

Wakazi wa kata ya Mwandeti wakimsikiliza mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi Dkt Johannes Lukumayi

Pia aliwataka watalaamu wa sekta mbalimbali ambao wameajiriwa na Serikali wanatakiwa watembelee miradi na kisha kubaini changamoto mbalimbali ambazo zinasababisha miradi hiyo kushindwa kukamilika kwa wakati 


Alihitimisha kwa kuwataka wananchi washirikiane kuleta maendeleo bila itikadi ya kisiasa lakini pia kushirikiana na wawekezaji ambao wanawekeza miradi mbalimbali ndani ya Kata hiyo 


Nao wananchi wa kata hiyo walisema kuwa wanaiomba Serikali iweze kuwatatulia matatizo mbalimbali ambayo yanawakabili 


Waliomba kuboreshewa zaidi kwenye sekta ya afya,elimu pamoja na miundombinu ambayo ni muimu kwenye sekta ya maendeleo hapa nchini 


Mwisho

No comments: