SEIF TAKAZA IRAMBA
maipacarusha20@gmail.com
Mwenge wa Uhuru umewasili katika Wilaya ya Iramba ukitokea Halmashauri ya Manispaa ya Singida na kupokelewa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Alhaj Suleiman Mwenda kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Singida Godwin Gondwe
Makabidhiano hayo ya Mwenge wa Uhuru yamefanyika tarehe 24 Julai, 2026 katika Uwanja wa Mcharukoni uliopo kijiji cha Ndulungu.
Akipokea Mwenge wa Uhuru, Alhaj Mwenda amesema kuwa Mwenge wa Uhuru utakimbizwa umbali wa kilometa 174.5 ndani ya Wilaya ya Iramba na utapitia jumla7 ya miradi nane (8) ya maendeleo yenye jumla ya thamani ya shilingi bilioni 12.5. kati ya miradi hiyo, minne (4) itazinduliwa, mitatu (3) itawekewa mawe ya msingi, huku mradi mmoja (1) ukitembelewa na kukaguliwa.

No comments:
Post a Comment