DC MWENDA AWAPONGEZA TRA KWA KUVUKA LENGO LA UKUSANYAJI WA MAPATO WILAYANI IRAMBA - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Friday, 14 August 2026

DC MWENDA AWAPONGEZA TRA KWA KUVUKA LENGO LA UKUSANYAJI WA MAPATO WILAYANI IRAMBA

 


NA SEIF TAKAZA IRAMBA
 
maipacarusha20@gmail.com


MKUU wa Wilaya ya Iramba,  Mkoani Singida Alhaj . Suleiman Mwenda,  ameipongeza Mamlaka ya Mapato (TRA)  kwa kukusanya  zaidi ya shilingi bilioni tano kwa mwaka wa fedha  2025 /2026 Wilayani Iramba.

Ametoa Pongezi hizo jana katika kikao  kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba  mjini Kiomboi.

Katika kikao hicho,  Alhaj Mwenda   amesema amefurahishwa na taarifa ya TRA baada ya kusikia   imevuka lengo kwa kukusanya asilimia 122.7

“Ngugu zangu natoa pongezi za dhati  kwa Watumishi  wa TRA,kwani wamejitahidi  katika ukusanyaji wa mapato    hadi kuvuka lengo.” Alisema

Naiomba Halmashauri ya Wilaya hii ifanye kama wanavyofanya TRA ili Wilaya yetu iwe na mapato ya kutosha kwa ajili ya Maendeleo ya Wilaya yetu " Amesema Mwenda

Kwa upande wake, Afisa Msimamizi wa Mapato TRA Wilaya ya Iramba  Herel Peter Akyoo amesema lengo la Ukusanyaji  mapato mwaka wa fedha 2025/2026 ilikuwa kukusanya shilingi bilioni 4,355,403,306.07

"Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya  lengo letu ilikuwa kukusanya zaidi ya bilioni tano lakini kwa sasa tumekusnya zaidi  na kupata ziada  shilingi 987,261,575.13 ambapo ni sawa na asilimia 122.7""alisema Akyoo.

Kwa Upande wa Tanesco  Meneja wa Shirika hilo Uswege Abel Mwasaguti amsema vijiji vyote 70 vya Wilaya hiyo vina umeme  na mitaa nane  ambapo Wilaya ina vitongoji 393 hivyo katika Wilaya hiyo vitongoji 260 vina umeme na vitongoji 133 havina Umeme lakini kwa sasa vitongoji 65 vinashughulikiwa na wakandarasi wako kazini.

Kikao kazi hicho kililenga kufanya tathmini ya utekelezaji wa majukumu ya Taasisi, Idara na Vitengo kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Kujadili muelekeo na mpango wa Taasisi hizo kwa mwaka wa fedha 2026/2027 na miaka mitano ijayo pamoja na kusikiliza na kutatua changamoto  za watumishi.

 MWISHO.

No comments: