GODBLESS LEMA akizungumza na Waandishi wa Habari mapema leo |
Mwandishi wetu, Maipac
maipacarusha20@gmail.com
Mwenyekiti Chadema Kanda ya Kaskazini Godbless Lema amemuomba , Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuondoa Marufuku ya kuruhusu Tanzanite kuuzwa Arusha na miji mingine kwani Kuzuia ni Ujima.
Lema amesema hayo katika Mkutano wake na vyombo vya Habari Jijini Arusha Leo Machi 4,2023 na kueleza Kuuzwa Madini ya Tanzanite Katika Mjii wa Mererani Pekee ni kosa la Kimkakati na la Kibiashara.
Amesema kuwa ni wakati Sasa Serikali Kuruhusu Mfumo wa Biashara Huria kwa Madini ya Tanzanite Ili yapatikane kwa wepesi Ndani na nje ya Nchi .
Lema Ameitaka kudhibiti madini kutoroshwa serikali inatakiwa kuwa na utaratibu wa kutoa certificate maalum ya kuonesha madini halali.
Lema Amebainisha Kuwa Mfumo wa Soko Huria katika Uuzaji wa Madini ya Tanzanite Utaongeza Mapato ya Serikali na hivyo kuchangia Ukuaji wa Uchumi wa Nchi ya Tanzania.
Amesema kuwa Arusha Ni Jiji la kitalii hvyo Serikali inapaswa Kuruhusu Biashara hyo Kufanyika Arusha mjini kupitia Broka ambao Wana leseni za Kufanya Biashara hyo Ili kuwezeshaji upatikanaji wake kwa wepesi.
Amesema walioleta hoja ya Kuzuia biashara ya Tanzanite kufanyika nje ya Mererani wanamawazo ya ujima kwani duniani ya Sasa jambo hilo haliwezekani.
"Leo ulienda nchi za Afrika ya Kusini,Kenya Dubai utakuta Tanzanite lakini Arusha hakuna Tanzanite"amesema
No comments:
Post a Comment