Na: Mwandishi wetu, Arusha
maipacarusha20@gmail.com
Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania, Edward Ngoyai Lowassa amefariki dunia katika hospital ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, jijini Daresalaam alipokuwa anapatiwa matibabu.
Edward Lowassa alikuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa kipindi cha mwaka 2005 hadi 2008 na kuweka rekodi ya kuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Tanzania kujiuzulu wadhifa wake.
Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango akiwa Longido Mkoani Arusha ameutangazia umma kifo cha Waziri Mkuu Edward Lowasa kupitia Televisheni ya Taifa TBC 1.
Amesema kufuatia kifo hicho RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluh Hassan ametangaza siku Tano za maombolezo ambapo bendera zitapepea nusu mlingoti.
"Ndugu watanzania wenzangu Rais Samia Suluhu anatangaza kifo cha Waziri Mkuu mstaafu ambaye amefariki Leo saa nane mchana"amesema.
Amesema Lowassa amefariki akiwa anapatiwa matibabu JKCI kutokana na Ugonjwa kujikunja utumbo na matizo la mapafu
Amesema awali Lowassa alikuwa amepelekwa kwa matibabu nchini Afrika Kusini akitoka JKCI na baadaye alirejea tena hospital ya JKCI Hadi Leo alipofariki.
No comments:
Post a Comment