DC Rukia, atembelea na kukagua ujenzi wa hospitali Wilaya Mwanga, Chuo cha ufundi Veta - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Friday, 6 February 2026

DC Rukia, atembelea na kukagua ujenzi wa hospitali Wilaya Mwanga, Chuo cha ufundi Veta

 

Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Rukia Zuberi akiwa ameambatana na Kamati ya usalama ya Wilaya hiyo, kukagua majengo ya hospitali ya Wilaya hiyo.




Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Rukia Zuberi akikagua ujenzi wa chuo cha Veta kinachojengwa katika Wilaya hiyo.Kukamilika kwa ujenzi wa chuo hicho kutasaidia kuwajengea juzi mbalimbali vijana wa Wilaya hiyo ambapo pia itasaidia kutatua changamoto ya ajira.


Na Mwandishi Wetu, Mwanga


maipacarusha20@gmail.com


Mwanga: Mkuu wa Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro, Rukia Zuberi, ametembelea Hospitali ya Wilaya ya Mwanga ili kujionea maendeleo ya shughuli mbalimbali za ujenzi zinazoendelea katika hospitali hiyo.


Mkuu huyo amesema kukamilika kwa ujenzi wa hospitali hiyo kutapunguza kwa kiasi kikubwa adha iliyokuwa ikiwakabili wananchi wa wilaya hiyo, ambao walilazimika kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya.


Awali, wananchi wa Wilaya ya Mwanga walikuwa wakilazimika kwenda katika hospitali za rufaa na kibingwa zilizopo nje ya wilaya hiyo ili kupata huduma za afya, hali iliyosababisha usumbufu na gharama kubwa kwao.


Pamoja na mambo mengine ametembelea chuo cha ufundi Veta, kinachojengwa katika Wilaya hiyo, ambapo amesema kukamilika kwake kutasaidia kuwapatia vijana juzi mbalimbali zitakazowasaidia kujikwamua kiuchumi.

No comments: