Mbunge Ibraline aeleza chanzo cha ajali msafara wa PM, awashukuru wananchi wa Moshi. - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Sunday, 8 March 2026

Mbunge Ibraline aeleza chanzo cha ajali msafara wa PM, awashukuru wananchi wa Moshi.

 




Na mwandishi Wetu 


maipacarusha20@gmail.com 


Moshi: Mbunge wa Moshi Mjini (CCM), Ibrahim Shayo amewashukuru wananchi wa Jimbo hilo kwa kumwombea kufuatia ajali aliyopata Februari 18 mwaka huu akiwa kwenye ziara ya Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba akisema ajali hiyo ni mtihani wa Mwenyezi Mungu na kwamba haihusiani na mkono wa mtu.


Amesema chanzo cha ajali hiyo inatokana na tairi la mbele la gari walilokuwa wakisafiri kupasuka na  dereva kushindwa kulimudu gari hilo ambalo lilikuwa  katika spidi 160.


Mbunge huyo ameyasema hayo  leo, Machi 8, alipokuwa akizungumza na wananachi wa jimbo hilo katika viwanja vya stendi ya mabasi mjini Moshi.


Mbunge huyo pia aliwashukuru wananachi kwa dua zao na kueleza kuwa sasa yupo tayari kuchapa kazi na kutekeleza ahadi zake za kampeni.


Shayo aliongeza kuwa anaamini ajali hiyo ilikuwa mtihani wa Mwenyezi Mungu, na anashukuru kuwa amepata nafuu na anaendelea na kazi kama kawaida .


Mwisho.

No comments: