Na Queen Lema, Arusha
maipacarusha20@gmail.com
Wito umetolewa kwa wafugaji wa wilaya za Monduli na Longido kuhakikisha kuwa wanajumuika Kwa pamoja kwenye mradi wa hewa ya Carbon ya Udongo
Mradi huo unaotekelezwa na Soil for the future umeweza kutekelewa kwenye vijiji zaidi ya 15 kutoka katika wilaya za Monduli pamoja na Longido mkoani Arusha
Akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na mradi huo Bw Richard Ndaskoi alisema kuwa mradi huo umekuwa na faida kubwa sana kwa wafugaji wa wilaya hizo
Akitaja faida ni pamoja na kuwa na maongezeko ya uuzaji wa Carbon lakini pia hata uhakika wa malisho ambayo yanaweza kuwanufaisha wafugaji wenyewe
"Huu mradi unasaidia sana kwa mfano hii carbon ya udongo inatokana na mimea michanga na mifugo inatakiwa Ile kiasi lakini ile mifugo ikishakula Kwa kiasi inaacha inaenda sehemu nyingine ambayo ina malisho hapo sasa mifugo inakuwa na uhakika kabisa wa malisho"aliongeza
Katika hatua nyingine alidai kuwa wafugaji wa vijiji vya wilaya hizo mbili wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanakimbilia mradi huo kwani mbali na elimu pia wataweza kuwanusuru mifugo Yao hasa nyakati za ukame
"Ukame ulitokea wiki chache hapa Arusha lakini vijiji ambavyo vimejiunga na mradi huu mifugo Yao ilizoroteka tu na haikufa lakini walibaki hai sasa basi nawakaribisha sana waje kwenye mradi huu' alisema
Alisema kuwa mradi huo katika wilaya hizo mbili wameweza kutekeleza mradi huo Kwa asilimia 50 ingawaje walitamani Mpaka sasa wawe wamefikia kiwango kikubwa cha utekelezaji lakini bado wamekutana na changamoto mbalimbali
Alitaja changamoto hiyo kuwa ni pamoja na kuwepo na baadhi ya watu wasio na nia Njema na mradi huo wa hewa ya Carbon ya Udongo.
Ndaskoi Alisema kuwa kundi Hilo la watu wamekuwa wakiwarubuni baadhi ya vijiji na kuwaaminisha kuwa hawapaswi kujiunga na mradi huo kwani wanaweza kuibiwa ardhi Yao Jambo ambalo sio la kweli kabisa
"Mimi nataka kusema kuwa huu mradi hauna nia ya kunyanganya Mtu ardhi yake Bali tunawawezesha kwa kiasi kidogo alafu wao sasa watakuja kuzalisha wwenyewe na kuuza mapato yatarudi kwenye jamii "aliongeza


No comments:
Post a Comment